Bayern Munich inaweka matumaini yake kwa nahodha wa Uingereza Harry Kane kuirejesha timu yenye kigugumizi katika msimu wake mbaya zaidi katika muongo mmoja kwa magwiji hao wa Ulaya.

Taji la 11 mfululizo la Bayern la Bundesliga lilishindwa kufua dafu juu ya nyufa za timu ambayo bado haijaboreka tangu kuwasili kwa mkufunzi Thomas Tuchel mnamo Machi.

Usajili wa wiki jana wa Kane kwa euro milioni 100 ($109 milioni) kutoka Tottenham ya Ligi Kuu ya Uingereza ulivunja rekodi ya uhamisho ya klabu hiyo ya Ujerumani.

Mkataba huo pia ulivunja ahadi ya muda mrefu kutoka kwa bosi wa zamani Uli Hoeness kwamba klabu “haitanunua mchezaji kwa milioni 100 hata kama ningekuwa na pesa.”

Lakini iwapo Kane mwenye umri wa miaka 30, ambaye anawasili baada ya kufanikiwa lakini bila taji lolote kaskazini mwa London, anaweza kuwa mwokozi wa Bayern bado haijaonekana