JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
TAARIFA KWA UMMA
UFAFANUZI KUHUSIANA NA EL NIÑO
Dar es Salaam, 03 Mei, 2023:
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inapenda kutoa ufafanuzi juu ya uwepo wa
hali ya El Niño na uhusiano wake katika mienendo ya mvua nchini.
El Niño ni mfumo wa hali ya hewa unaosababishwa na uwepo wa joto la bahari la juu
ya wastani katika eneo la kati la kitropiki la bahari ya Pasifiki.
Hali hii kwa kawaida
huambatana na vipindi vya mvua kubwa vinavyoweza kusababisha mafuriko.
Mamlaka ya Hali ya Hewa, ilifuatilia mifumo ya hali ya hewa wakati wa maandalizi ya
msimu wa mvua za Masika (Machi hadi Mei), 2023 na inaendelea kufuatilia mifumo
hiyo ikiwemo El Niño.
Aidha, kama ilivyoanishwa kwenye taarifa ya utabiri wa msimu wa mvua za Masika
iliyotolewa terehe 22 Februari, 2023 viashiria hivyo vilikuwa vinaonesha mvua hizi
kuanza mwezi Machi, katika maeneo mengi na kuisha katika wiki ya nne ya mwezi Mei
2023 katika maeneo mengi ingawa mwendelezo wa mvua za nje ya msimu ulitarajiwa
mwezi Juni 2023 katika maeneo machache.
Maandalizi ya Utabiri wa msimu wa Kipupwe (Juni hadi Agosti, 2023) unaendelea na
taarifa yake inatarajiwa kutolewa mwishoni mwa mwezi Mei.
Kwa taarifa hii wananchi wanashauriwa kuendelea kuzingatia taarifa za hali ya hewa
zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania sambamba na kutafuta, kupata
na kuzingatia ushauri wa wataalam katika sekta husika ili kupunguza athari
zinazotokana na hali mbaya ya hewa.
Imetolewa na:
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania
0 Comments